Sijasoma nimeolewa na msomi ila ananitesa na elimu yake
Nilipo maliza form four matokeo yangu yalitoa vibaya hivyo nikaamua nirudie ili kutafuta credit, niliendelea na uvumilivu huo, nikalipa kila kitu kwaajili ya mtihani wangu, wakati naendelea na maandalizi nilipata mchumba akaniambia ndakuoa, kabla ya miezi miwili kwenda kwenye chumba cha mtihani nikaonekana nina ujauzito wa huyo mwanaume, kwa mila zetu za kichaga lazima ufukuzwe nyumbani, nikafukuzwa nyumbani nikaenda kwa huyo mwanaume, nikasahau kabisa elimu yangu, tukaanza maisha, yeye alikuwa amesoma na alikuwa anafanya kazi ya ufamasia. Nikajufungua mtoto wa kwanza kabla mtot huyo hajaacha kunyonya nikapata mimba mingine akiwa na miezi mitano, mume wangu akanishauri tuitoe hiyo mimba nikakataa sana sana, akanibembeleza maana nilikuwa naoogopa kufa wengine wanapotoa mimba wanafia hiyo hiyo, siku moja asubuhi niliamka vibaya mwili haukuwa vizuri sasa kwa kuwa yeye ni daktari akasema atanihudumia bila kujua dawa anazo tumia kunitibu kumbe ni dawa za kutolea mimba, ile mimba ikatoka, ...