Posts

Showing posts from 2017

Nimeathirika kisaikolojia baada ya kuachwa nimeapa siji kuolewa tena

Image
Nilikuwa na mpenzi wangu ambaye tulianza naye shule ya msingi darasa la tano, wakati huo ulikuwa utoto mwingi, endapo hatukuwahi kulala, lakini tuliahidiaana kwamba tutapendana na hatuta achana. Alinipenda kweli kweli na mimi nilimpenda kweli kweli, ila tulikuwa hatuchezeani. Nilimkubali katika ahadi zake, hadi wazazi wetu walijua kwamba mimi na yeye tutakuja kuwa mme na mke, miaka mingi ikapita, tuka maliza shule ya msingi na sekondari, bado mahusiano yalikuwepo na yalikuwa na nguvu. Migogoro ilianza pale ambapo matokeo ya kidato cha sita yalipotoka, yeye alichaguliwa maana ufalu wake ulikuwa mzuri, mimi sikuchaguliwa maana ufaulu wangu haukuwa vizuri. Yeye akaenda UDOM mimi nikabaki nyumbani, nikijua ndugu yangu baada ya kumaliza ahadi yetu itatimia, kila rikizo bado alionesha msimamo kwaajili yangu kwamba ananipenda na ataishi na mimi, alipofika mwaka wa mwisho wakati na mimi najiandaa kwamba sasa naenda kuolewa, huyo mme mtarajiwa. Siku hiyo nilienda kutembelea kwao, nik...

Sijasoma nimeolewa na msomi ila ananitesa na elimu yake

Image
Nilipo maliza form four matokeo yangu yalitoa vibaya hivyo nikaamua nirudie ili kutafuta credit, niliendelea na uvumilivu huo, nikalipa kila kitu kwaajili ya mtihani wangu, wakati naendelea na maandalizi nilipata mchumba akaniambia ndakuoa, kabla ya miezi miwili kwenda kwenye chumba cha mtihani nikaonekana nina ujauzito wa huyo mwanaume, kwa mila zetu za kichaga lazima ufukuzwe nyumbani, nikafukuzwa nyumbani nikaenda kwa huyo mwanaume, nikasahau kabisa elimu yangu, tukaanza maisha, yeye alikuwa amesoma na alikuwa anafanya kazi ya ufamasia. Nikajufungua mtoto wa kwanza kabla mtot huyo hajaacha kunyonya nikapata mimba mingine akiwa na miezi mitano, mume wangu akanishauri tuitoe hiyo mimba nikakataa sana sana, akanibembeleza maana nilikuwa naoogopa kufa wengine wanapotoa mimba wanafia hiyo hiyo, siku moja asubuhi niliamka vibaya mwili haukuwa vizuri sasa kwa kuwa yeye ni daktari akasema atanihudumia bila kujua dawa anazo tumia kunitibu kumbe ni dawa za kutolea mimba, ile mimba ikatoka, ...

Mwanzo wa ndoa yangu

Image
Mimi kabla sijaolewa nilijua upendo ambao upo kipindi cha uchumba utaendelea hadi kipindi cha ndoa, lakini nikaja kuwa na mshangao baada ya mme wangu kuingia ndani ya ndoa. Maisha yalibadilika na kila kitu kikaenda kusiko takiwa, mume wangu alinikuta nimejitunza nilipokuwa kwetu tabia zangu zilimvuta kunipenda. Siku moja nilikuta nina dalili za magonjwa ya zinaa, nilipo amka asubuhi niliwaza sana nikasema hivi haya magojwa yanatoka wapi mbona mimi nimejutunza, sikujua nikasema inawezekana magonjwa yaha kuna njia nyingine ambayo yanaambukizwa, lakini nilienda kwa mtu ambaye ni mzima nikamweleza kile ambacho kinatokea kwenye mwili wangu, Yule mtu mzima akaniambia kweli wewe bado ni mtoto katika ndoa, magonjwa ya zinaa yanasababishwa na kujaamiana. Ukiona magonjwa kama hayo yameingia ujue kuna mmoja kati yenu si mwaminifu, akaniambia kama siyo wewe basi mumeo anatoka nje ya ndoa, niliposikia hayo moyo wangu uliuma sana kwa uchungu, nikawaza nakusema mimi narudi kwetu, kama mwanam...